Updated Jun 16, 2026 · v2 . 4 . 9
Nakala ya nyimbo za ibada za waadventista wasabato kwa lugha ya kiswahili.
Nyimbo za Kristo ni programu inayojumuisha mkusanyiko wa nyimbo 220 kutoka katika kitabu cha Nyimbo za Kristo cha kanisa la Waadventista Wasabato kwa lugha ya Kiswahili kama kilivyohaririwa na kuchapwa na TANZANIA ADVENTIST PRESS (TAP). Programu hii imeandaliwa kukuwezesha kumuamudu Mungu kwa njia ya uimbaji mahali popote na muda wowote, Nyimbo za kuburudisha, kutia moyo na kukufariji wakati wa huzuni. Sifa za program ni kama zifuatazo:- • Inahusisha eneo la utafutaji ambapo unaweza kutafuta wimbo kwa namba au kwa neno unalokumbuka liwe jina la wimbo kwa Kiswahili, kwa kiingereza au maneno yaliyo ndani ya wimbo. • Inakuwezesha kuweka nyimbo unazozipenda katika orodha tofauti na hivyo kuupata kwa urahisi wakati mwingine, pia unaweza kuuondoa pale unapoona inafaa. • Inakuwezesha kuona nyimbo kwa makundi. • Inakuwezesha kufuatilia wimbo kwa njia ya ala za sauti (thanks to hymnserve.com for the accompaniments). • Inakuwezesha kucheza ala ya wimbo hata usipokuwa kwenye programu • Inakuwezesha kuona wimbo unaocheza • Inakuwezesha kukuza ukubwa wa maandishi wa maneno ya wimbo kadri unavyoona inafaa. • Inakuwezesha kuona wimbo uliofunguliwa mara ya mwisho kwa kuuangaza. • Inakuwezesha kushiriki maneno ya wimbo na ndugu jamaa na marafiki kwa urahisi. • Inakuwezesha kubadili muonekano wa programu unaofaa katika mazingira ya Mwanga au Giza ili kuwezesha uono usioumiza macho.
6 years on Google Play
This app isn't currently appearing in any tracked top charts.